BILONEA na Mgombea Urais wa Marekani
kupitia chama cha Republican Donald Trump amemtaka kocha wa Arsenal
,Arsene Wenger kuondoka katika klabu hiyo kwa kuwa ameshindwa kuipa
mafanikio timu hiyo.
Trump ambaye anasifika kwa kuongea
sana,amesema kuwa toka klabu hiyo ilipopata mafaniko mwaka 2004 hadi
sasa hawajawai kufurahia uongozi wa Arsene Wenger katika klabu hiyo.Aidha,Trump
ameitaka bodi ya klabu ya Arsenal kumfukuza kocha huyo na kuhaidi kuwa
yupo tayari kuhusishwa katika malipo ya mshahara wa kocha mpya
atakayeleta mafaniko katika klabu hiyo hata kwa kipindi cha miaka 50
ijayo.
Amesema kuwa anashangazwa na kocha huyo
kuifanya Arsenal kama mali yake bila kujua kuwa mamilioni ya mashabiki
wa klabu hiyo duniani kote akiwemo yeye anaumia na matokeo mabovu ya
klabu hiyo.
“Mimi ni shabiki mkubwa
namba moja wa klabu hii ,kama mashabiki wengine wa Arsenal siridhishwi
na jinsi huyu kocha anavyoiongoza klabu yetu,haiwezekani klabu za
Manchester United na Chelsea zikawa zinapata ushindi wa nyumbani na
ugenini dhidi yetu,hata hawa Swansea ni timu ndogo sana lakini iweje
wapate matokeo dhidi ya timu imara kama yetu?
Trump ni shabiki wa kutupwa wa washika
bunguki hao,na amekuwa mmoja ya wahanga wa matokeo mabovu yanayoikabili
timu ya Arsenal kwa kipindi kirefu.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
TRUMP : WENGER AFUKUZWE KAZI HARAKA
Reviewed by Newspointtz
on
12:45:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment