WAZIRI
wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe ameuagiza Wakala wa Usajili,
Ufilisi na Udhamini (RITA) kusitisha mara moja usajili mpya wa
wadhamini wa asasi, vyama, misikiti na vikundi mbalimbali vya kijamii
kwa lengo la kufanya uhakiki wa uhalali wa kuwepo wa taasisi hizo
kisheria.
Ameagiza
kuwa uhakiki huo ukamilike ndani ya miezi mitatu (siku 90) kuanzia sasa
na orodha kamili ya wadhamini ikiwa ni pamoja na picha zao, anuani ya
posta na makazi, na taarifa nyingine muhimu za utambuzi wa taasisi hizo
mahali zilipo.
Taarifa hizo ziwasilishwe Rita na nakala wizarani kwa uhakiki na kumbukumbu.
Dk
Mwakyembe alitoa agizo hilo, alipokutana na watendaji na uongozi wa
Bodi ya Rita, Dar es Salaam jana kwa lengo la kuboresha utendaji wa
Wakala na kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano. Rita ina zaidi
ya wadhamini 5,000 walio kwenye vitabu vyao vya usajili.
Aidha,
Waziri huyo ameitisha kikao wiki ijayo cha mamlaka zote zinazohusika na
usajili wa vikundi vya kijamii, mashirika, kampuni na asasi mbalimbali
kwa lengo la kuimarisha taratibu za usajili na uendeshaji na kuboresha
mawasiliano baina ya vyombo vya usajili vya dola ili kulinda maslahi
mapana ya Taifa.
0 comments:
Post a Comment