Yanga imejiweka kwenye mazingira mazuri ya kufuzu kwenye hatua inayofuata baada ya ushindi wa ugenini wa magoli 2-1 dhidi ya APR kwenye uwanja wa Amahoro, Kigali, Rwanda.
Juma Abdul alianza kuifungia Yanga bao la kwanza dakika ya 20 kipindi cha kwanza.
Dakika ya 75 Thaban Kamusoko akafunga bao la pili akilitendea haki pande la Donald Ngoma kisha kupiga shuti akiwa ndani ya box na kuifungia Yanga bao la pili.
0 comments:
Post a Comment