Serikali ya Tanzania imewaagiza
mawakala wa Pembejeo za kilimo nchini kuhakikisha kuwa wanawafikishia
wakulima vocha za pembejeo za kilimo kwa wakati ili waweze kuzalisha
chakula kwa wingi na nchi kuwa na uhakika wa chakula.
Agizo hilo limetolewa na waziri wa
kilimo, uvuvi na mifugo Mwigulu Nchemba kufuatia malalamiko ya wakulima
wilayani Rungwe mkoani Mbeya ya kucheleweshewa pembejeo za kilimo
ikiwemo mbolea hali inayopelekea kuzalisha chakula kidogo tofauti na
matarajio
.Kumekuwepo
na malalamiko kutoka kwa wakulima dhidi ya mawakala wa Pembejeo za
kilimo mkoani Mbeya ya kupewa Vocha za Mbejeo baada ya msimu kuanza hali
inayopekea wakulima hao kuhisi watendaji na mawakala wana nia ya
kuhodhi pembejeo hizo.
Waziri Nchemba amesema wakulima
wanahitaji kuzalisha kisasa kwa kuzalisha chakula kwa wingi kwa kutumia
mashamba madogo na kuwa Serikali itahakikisha inawapatia mbegu bora ili
kutimiza adhma hiyo.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
WAZIRI WA KILIMO ATOA AGIZO VOCHA ZA PEMBEJEO
Reviewed by Newspointtz
on
07:23:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment