NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Waziri wa maji atumbua jipu LA DAWASCO

 

Waziri wa maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge ameiagiza bodi ya kampuni ya maji safi na taka Dar es salaam (DAWASCO kuwasimamisha kazi watendaji tisa wa mamlaka hiyo pamoja na aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Injinia Jackson Midalla kupisha uchunguzi uliosababisha hasara ya kiasi cha shilingi bilioni.2.9 ambazo kampuni ya ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo haraka Strabag ilipaswa kulipa.

Agizo hilo limetolewa jijini Dar es salaam na Mhandisi Lwenge alipokuwa akizungumza na watendaji wa DAWASCO ofisini kwao ambapo amesema katika uchunguzi wa awali, imeonekana kiasi hicho cha fedha kilitakiwa kulipwa na kampuni ya stragbag kwa ajili ya matumizi ya maji katika ujenzi wa barabara lakini hazijaingia na kubaini kuwa wapo baadhi ya watendaji waliohusika kwa namna moja ama nyingine katika suala hilo.

Mhandisi Lwenge amewataja watendaji hao ambao wanatakiwa kusimamishwa kazi mara moja na kutafutwa popote alipo aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo injinia Jackson Midalla wakati huo.

Aidha, ameitaka bodi hiyo kufanya uchunguzi wa haraka na kuhakikisha kampuni ya strabag inalipa kiasi hicho cha fedha ndani ya siku 14 vinginevyo hatua za kisheria zitafuata na kufuatilia akaunti za makampuni na viwanda vikubwa ili kujiridhisha kama zinalipia huduma ya maji.

 

 

chanzo>mtembezi 

 

 

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment