NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Afisa Mtendaji Atumbuliwa Kwa wizi wa Madawati


Paul Simwela Ofisa Tarafa wa Mkunya


MTWARA Na; Sigfrid Bina 

Maafisa Watendaji wa Serikali wa kata na vijiji Wilayani Newala Mkoani Mtwara wametakiwa kutojichulia maamuzi binafsi katika matumizi ya mali za umma kwani kufanya hivyo ni kinyume cha utaratibu wa utendaji. 

Hayo yamebainisha jana tarehe 6 April 2016, na Ofisa Tarafa ya Mkunya Bwana Paul Simwela ofisini kwake mjini Newala wakati anatolea ufafanuzi juu ya hatua zilizochukuliwa kwa Ofisa Mtendaji wa kijiji cha Mnalale Bw. Awadhi Rashid Hulewa baada ya kuchukuwa madawati shule bila ruhusa na kutengeneza meza za ofisi ya kijiji ambazo nazo aliziuza. 

Simwela amesema kitendo hicho hakikubaliki kwa kiongozi wa umma kuwa kiongozi wa kutenda mauovu kwa kuhujumu maendeleo ya wananchi wanaowatumikia na kurudisha nyuma juhudi za serikali za kupambana na umasikini hasa ukizingatia sekta hiyo ya elimu inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo upungufu wa madawati. 

Katika hatua ya kukomesha tabia hiyo, mtendaji huyo amevuliwa madaraka, ameamriwa kurejesha madawati aliyoyachukua ndani ya mwezi huu wa nne, vinginevyo atafikishwa mahakamani, hatua nyingine ni pamoja na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mcholi moja kutakiwa ndani ya siku 5 ahakikishe amechagua mtendaji mwingine kutoka ndani ya wajumbe 25 wa halmashauri ya kijiji. 

Ofisa Mtendaji huyo amekiri kuchukua madawati hayo mali ya shule ya Msingi Mnalale Kata ya Mcholi 1 wilayani Newala na kwenda kubadilisha matumizi kwa kutengeneza Meza mbili za ofisi ya kijiji ambazo pia aliziuza kwa Bw. Nuru Maneno na Bw. Kabunda wakazi wa Mcholi Godauni kwa Tsh, 25,000/= kwa meza zote. 
Hulewa amesema alichukuwa mbao hizo na kuahidi kuzirejesha baadae hivyo japo na kukiri kuchukua bila taarifa lakini lengo lake ni kuzirejesha baada ya ofisi kupata fedha ya kununulia thamani hizo. 

Fundi seremala aliyefanya kazi hiyo Mustapha Hassan amesema meza hizo zilitumia mbao za madawati manne na zingine zilibaki, ambapo Mwalimu mkuu wa Shule hiyo Alfani Mussa Mohamed amesema madawati yaliyopotea ni 10 na shule yake ilikuwa inakabiliwa na upungufu wa madawati 25 hivyo kuongeza ukubwa wa tatizo. 

Aidha pia Mwalimu mkuu huyo amebainisha kuwa wizi huo uliotokea wakati wa likizo ya mwezi December ambapo baada ya kufungua shule ndipo walibaini tatizo hilo ikiwa pamoja na upotevu wa Betri 2 za Solar shuleni hapo msaada wa 21st Century, Kitanda kimoja na magodoro 2 huku wizi huo wa Kitanda na magodoro ukihusishwa na mtendaji huyo ambapo kesi yake ipo kituo cha Polisi Newala. 

Tuhuma zingine zinazomkabili ni kujichukulia maamuzi ya kuandika Muhutasari kwa Ofisa Ushirika wilayani hapa wa kijiji hicho kujitoa katika chama cha msingi TUYANGATANE na kukipa hasara ya Tsh, 500,000/= kutoka kwenye chama hicho fedha za mgao wa chama kwa vijiji vinavyohudumia uamuzi ambao hakushirikisha wananchi na viongozi wengine wa halmashauri ya kijiji.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment