BENKI ya Dunia imepanga kuisaidia
Tanzania katika jitihada zake za kuboresha utendaji wa Idara ya Mahakama
kwa lengo la kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kusogeza haki jirani
zaidi na wananchi.
Hatua hiyo ilifikiwa jijini Washington,
Marekani jana baada ya Bodi ya Juu ya Wakurugenzi ya Benki ya Dunia
kupitia taasisi yake inayoshughulikia utoaji wa misaada na mikopo nafuu
kwa mataifa masikini duniani (IDA) kuidhinisha mkopo nafuu wa Dola za
Marekani milioni 65 kwa Tanzania ili kuweza kusaidia Mpango wa Maboresho
ya Mhimili wa Mahakama ili kuongeza ufanisi, uwazi na urahisi wa kupata
huduma za Mahakama.
Mradi huo mpya umeainishwa katika
Mpango wa Maendeleo wa Taifa na pia katika Mpango Mkakati wa Maboresho
ya Idara ya Mahakama wa mwaka 2015-2025.
Kupitia mipango hiyo, Serikali imelenga
kuboresha maisha ya wananchi kwa kuboresha mazingira ya biashara na
uwekezaji, kuongeza uwazi, uwajibikaji na kupunguza umasikini.
Mpango wa Maboresho katika Mhimili wa
Mahakama utaongeza ufanisi katika utekelezaji wa vipaumbele vya taifa
kwa kusaidia kuboresha utoaji wa huduma na pia kuongeza wigo wa
upatikanaji wa haki.
“Kuna idadi kubwa sana ya Watanzania
ambao kwao upatikanaji wa huduma za kimahakama ni mgumu kutokana na
ugumu wa gharama, lakini haipaswi kuwa hivyo kwa vile ni suala muhimu
kwa ustawi wa maisha ya jamii na maendeleo ya watu wake,” alisema Bella
Bird ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia katika mataifa ya
Tanzania, Burundi, Somalia na Malawi.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
Benki ya Dunia kuipa Tanzania Dola millioni 65
Reviewed by Newspointtz
on
07:00:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment