Hitmaker wa Fundi Mh Temba ameiambia
mtembezi.com kuwa ameamua kufanya video yake ya wimbo wa Fundi na
muongozaji Hanscana kwasababu ni muongozaji anayechipukia kwa kasi huku
akiwa na connections kubwa za nchi za nje, hivyo anaamini kuwa Hanscana
ndiye muongozaji bora kwa sasa.
Vilevile Mh. Temba amejibu swali
lililoulizwa na wengi kuhusu sauti za kike zinazo sikika kwenye nyimbo
hiyo na kueleza kuwa moja ya sauti katika nyimbo hiyo zimeingizwa na
mrembo Jokate Mwegelo.
Akizungumzia ukaribu wake na Jokate Mh.
Temba amesema kuwa Jokate ni rafiki yake wa karibu ndio maana imekuwa
rahisi kufanya kazi nae, hivyo mashabiki wake watarajie mengi kutoka
kwake.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
Mh Temba awachana Hanscana ,Jokate(+Audio)
Reviewed by Newspointtz
on
06:57:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment