NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Hospitali za Jakaya Kikwete, Mkapa kutibu wagonjwa wote wa Figo na Moyo nchini


SERIKALI imesema kwa sasa hakuna mtu yoyote ambaye ataenda kutibiwa nje ya nchi kutokana na magojwa ya figo na moyo.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alipokuwa fanya ziara ya maendeleo katika hospitali ya kisasa ya Benjamini Mkapa ambayo inahusika na matibabu ya magonjwa ya figo iliyopo katika chuo kikuu cha Dodoma mjini.

Majaliwa alisema sababu za kutokuwepo kwa wagonjwa kutibiwa nje ya nchi ni kutokana na kuwa na hospitali za kisasa ambazo zipo nchini.

Mbali na kuwepo kwa hospitali za kisasa sambamba na vifaa vya kisasa alisema wapo madaktari bingwa na wazuri ambao kwa sasa wanazalishwa hapa nchini.

Katika ziara hiyo akizungumza na waandishi wa habari pamoja na watumishi alisema kwamba kwa sasa si matibabu ya figo pekee bali hasha figo kutafanyikia hapa nchini badala ya kwenda nje.

“Kwa sasa hakuna mtu ambaye ataenda kutibiwa nje ya nchi kwa ugonjwa wa figo wala moyo, wagonjwa wote watatibiwa hapa ndani na si kutibiwa tu bali hata kubadilisha figo itafanyika hapa nchini.

“Serikali kwa sasa imeweza kuimalisha huduma hiyo kwa kuweka mashine na vifaa vya kisasa katika hospitali ya Rufaa ya Muhimbili pamoja na hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo hapa (UDOM)”.alisema Majaliwa.

Alisema kutokana na kuimalisha uwezo mkubwa wa matibabu alisema kwa sasa wagonjwa kutoka nchi nchi jirani kama vile, Malawi,Msumbiji,Komoro,Waganda na Wakenya wanatibiwa nchini hapa.
Mbali na hilo Majaliwa ameagiza hospitali nchini kuacha kuhamisha vifaa vya hospitali za umma kwenda katika hospitali binafsi.

Alisema kwa sasa Hospitali ya Benjamini Mkapa ina vifaa vingi vya kisasa vyenye uwezo mkubwa ambavyo kwa sasa vinafanya kazi ya kutoa huduma ya matibabu ya ikiwemo ya figo, moyo na kansa.

Alisema kuna kila sababu ya kupunguza wimbi la kutoa vifaa vya serikali kupeleka katika hospitali binafsi. 

Sifikirii kwa malengo mliyonayo hapa mtatoa vifaa na kupeleka katika hispitali binafsi.
Aidha, Majaliwa alisema kutokana na uwezo na ukubwa wa vifaa katika hospitali hiyo imebidi kuvifanyia marekebisho vyumba kwa kuviimarisha ili kuwezesha vifaa hivyo kuingia kwenye vyumba husika.

Akitoa ufafanuzi zaidi Mjaliwa alisema kwa sasa mkandarasi anayefanya ukarabati na kujenga vyumba vya kuwekea vifaa vya tiba anatakiwa kuongezewa fedha na  maandiko yameaandaliwa kwa ajili ya kupelekwa bungeni ili kupata fedha.

Kutokana na baadhi ya vifaa kuhifadhiwa nje ya vyumba, Majaliwa aliwataka viongozi wa hospitali hiyo kuvilinda vifaa hivyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee, Dk Khamisi Kigwangalla, alisema Wizara yake inataka kufuta bajeti kwa ajili ya matibabu ya nje ya nchi na badala yake fedha hizo zitaelekezwa katika vituo husika vya kutolea huduma za matibabu.

Aidha badala yake kazi hiyo ya kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi itafanywa na hospitali za kisasa zilizopo nchini.

Hata hivyo serikali kupitia Wizara yake itaondoa kabisa jukumu la kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi na badala yake kazi hiyo itafanywa na hospitali za ndani.

Pia hospitali za kisasa ambazo zipo ndani ya nchi ndizo zitakazo toa kubali cha kupeleka wagonjwa nje ya nchi pale tu watakapoona kuwa wao wameshindwa kutoa huduma ya tiba kwa mgonjwa husika.

DSC_9884Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee, Dk Khamisi Kigwangalla akisalimiana na uongozi wa Hospitali ya Kisasa ya  Benjamini Mkapa iliyopo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)  wakati wa tukio hilo..
DSC_9912Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akisalimiana na Madaktari wa Hospitali ya Kisasa ya Mkapa wakati akiwasili kukagua Hospitali hiyo.
DSC_9913Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee, Dk Khamisi Kigwangalla akijadiliana jambo na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati wa ukaguzi wa Hospitali ya kisasa ya Mkapa iliyopo UDOM.
DSC_9914IMGS0780Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua mashine ya MRI ambayo inaendelea kufungwa katika jengo la Hospitali ya Kisasa ya Mkapa iliyopo UDOM.
DSC_9920Mashine hiyo ya MRI ambayo inaendelea kufungwa katika jengo hilo la Hospitali ya Kisasa ya Mkapa.DSC_9923Kaimu Mkuu wa Hospitali hiyo Profesa Gesai akimuonyesha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa namna ya uimala wa jengo hilo pindi watakapofunga vifaa vya kisasa  vya kutibu magonjwa mbalimbali.
DSC_9925
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia chumba cha CT-SCANA ambacho kinatarajiwa kukamilika hapo baadae 
IMGS0812 DSC_9938Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee, Dk Khamisi Kigwangalla akifafanua jambo kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa juu ya Wizara ya Afya ilivyojipanga kuiendesha Hospitali hiyo ya kisasa ya Mkapa ambayo inamiliki na Wizara kwa asilimia mia moja.
DSC_9942Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akitoa maagizo kwa Naibu Waziri wa Afya namna ya kuindesha Hospitali hiyo pamoja na masuala mbalimbali ya kitaalam
DSC_9947Mkurugenzi wa Tiba wa Wizara ya Afya, Dk. Magreth Mhando akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu Kasim Majaliwa katika tukio hilo la ukaguzi wa jengo hilo la kisasa la Hospitali ya Mkapa.
DSC_9970Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee, Dk Khamisi Kigwangalla akito maelezo ya kitaalam kwa Waziri Mkuu Kasim Majaliwa walipotembelea chumba cha vipimo
DSC_9988Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akitoa maagizo kwa Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla na watendaji wa Hospitali hiyo ya Mkapa wakati wa kuondoka baada ya kumaliza shughuli ya ukaguzi na kuangalia maendeleo ya ke. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog-DODOMA).
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment