NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Kabla ya kuwakabili Waarabu Mingange azipa somo Yanga ,Azam

Meja mstaafu Abdul Mingange-Kocha Ndanda FC
Meja mstaafu Abdul Mingange-Kocha Ndanda FC
Wawakilishi wa tanzania katika michuano ya kimataifa Young Africans pamoja na Azam  FC wametakiwa kujituma na kujitolea kwa asilimia 100 katika michezo yao ya mwishoni mwa juma.
Kocha mkuu wa Ndanda FC ya Mtwara Meja mstaafu Abdul Mingange amevitaka vilabu hivyo kupambana kutokana na wapinzani wa vilabu hivyo kuwa na uzoefu mkubwa kwenye mashindano hayo.

“Timu zote mbili zinacheza dhidi ya timu ngumu kwasababu hizo timu zinajua faida za mashindano haya kuanzaia wachezaji, viongozi wote wanajua faida ya mashindano hayo hilo la kwanza. Jambo la pili ni kwamba hizi timu hazijajengeka kwa muda mfupi zimejengwa kwa muda mrefu.

 Nataka nizungumzie Yanga, Pluijm ndiyo ameanza kujenga timu ambaye anataka timu iwe ya kimataifa zaidi lakini hajafikia hapo kwasababu bado kuna mapungufu mengi kwenye timu”.

“Al Ahly ni timu ambayo imelelewa kucheza mashindano makubwa hasa ukiangalia historia yao wameshachukua mara 8 kombe la Afrika wakati Yanga hawajawahi kufika hata nusu fainali. Kwahiyo si mchezo rahisi kama watu wanavyofikiria, kuwatoa waarabu kwenye mechin mbili siyo kitu rahisi Yanga wanakazi ya kufanya”.

“Mechi zao walizocheza kwenye michuano ya kimataifa bado hawajacheza vizuri, watu wanaangalia matokeo hawaangalii timu inavyocheza. Nikiipima na mechi ya Al Ahly naona shughuli ipo”.

“Azam tok alivyo rudi Stewart Hall ilinivutia ilivyocheza Kagame lakini kile kiwango kinazidi kupotea sasa inawezekana wachezaji wametumika sana au mwalimu inabidi abadilishe mtazamo wake kwenye timu kwasababu hata mechi wanazocheza kwenye ligi hawajacheza vizuri bado.

Ukiangalia mechi ya mwisho dhidi ya Bidvest Wits kama wasingecheza kwenye jua kali Azam wangepoteza mchezo ule lakini wapinzani wao walizidiwa sana na hali ya hewa”.

“Lakini jambo la mwisho wachezaji wanatakiwa kujitoa, moja ya tatizo ninaloliona kwa wachezaji wetu wa Tanzania ni kutojitolea kwa asilia mia 100 wenzetu wanajitolea kwa asilimia zote. Kwahiyo kama wachezaji wetu watajitolea ninauhakika timu hizi wanaweza kuzitoa”.

“Mpira unasema 50% ni spirit, unaweza kuishinda timu ambayo ina tactical, technical na physical approach nzuri ndiyo maana unakuta Yanga bado inafungwa na Coastal Union”.

Yanga wanaocheza michuano ya klabu bingwa Afrika watacheza Jumamosi dhidi ya Al Ahly kwenye uwanja wa taifa huku Azam FC wanaocheza kombe la shirikisho wakikipiga dhidi ya Esperance kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment