Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye amelihasa jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) kujenga uzalendo ndani ya jeshi letu kupitia michezo mbalimbali ndani ya jeshi hilo.

Waziri Nape ameyasema hayo wakati wamakabidhiano ya Ulingo wa Kisasa wa Ngumi kwa Jeshi hilo ili wautumie kwa ajili ya maandalizi mbalimbali ya mchezo wa ngumi kwani Serikali imeona ni sehemu salama zaidi na nidhamu ya kuutunza ipo na hata pale utapohitaji kakutumika kwingine uchukuliwe na kurudishwa jeshini hapo kwani jeshi hilo limeleta heshima kubwa ya michezo nchini na kulifanya Baraza la Michezo ya Majeshi (BAMMATA) kuimarika zaidi.

“Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limekuwa na mchango mkubwa sana katika michezo hapa nchini na limetuletea sifa kubwa sana kwetu na hivyo hatukuwa na shaka tulipoletewa ombi la ulingo huu. Ulingo huu utumike vyema na ulete heshima hapa nchini,”alisema Nape.

Aidha Waziri Nape alitoa rai kwa jeshi hilo kurudisha michezo jeshini kwani inajenga uzalendo na kuimarisha umoja,undugu na urafiki. Waziri huyo pia alikazia kuwa wizara yake itaendelea kushirikiana na jeshi hilo katika michezo mbalimbali nchini.
Na Daudi Manongi
4785-nape akiongea na brigadia
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akizungumza jambo na Mkuu wa Mafunzo na Operesheni jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ), Meja Jenerali Issa S. Nassoro wakati wamakabidhiano ya ulingo wa Ngumi leo jijini Dar es Salaam.
4788-nape na wenyeji
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (wa pili kushoto) akiwa na Mkuu wa Mafunzo na Operesheni jeshi la wananchi Tanzania, Meja Jenerali Issa S. Nassoro (wa kwanza kushoto) wakati wa makabidhiano ya Ulingo wa Ngumi uliotolewa na Wizara hiyo kwa jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ). Wengine pichani ni Brigedia Jenerali Martin Busungu ambaye ni mkurugenzi wa michezo jeshini (wa pili kulia) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo wizara ya  Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw.Alex Nkenyenge.
4860-nape akimvisha medali
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akimvisha medali bondia wa jeshi kama moja ya ishara ya ufunguzi wa ulingo wa ngumi waliopewa na wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuimarisha mchezo wa ngumi jeshini na nchini kwa ujumla kwani ulingo huo utatumiwa na baraza la Michezo ya majeshi kujiimarisha katika mchezo huo. Wengine pichani ni Mkuu wa Mafunzo na Operesheni  JWTZ,  Meja Jenerali Issa S. Nassoro (wa kwanza kushoto).
IMG_4814
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akimkabidhi Mkuu wa Mafunzo na Operesheni JWTZ,  Meja Jenerali Issa S. Nassoro ulingo wa Ngumi wa kisasa ambao wizara ilipewa na Serikali ya China kwa ajili ya maendeleo ya ngumi nchini. Wizara imeamua kuwapa jeshi kwa kuwa ni sehemu salama na watakuwa na nidhamu ya kuutunza na pia ulingo huo utaimarisha Baraza la Michezo ya Majeshi Tanzania (BAMMATA). Wengine pichani ni Brigedia Jenerali Martin Busungu ambaye ni mkurugenzi wa michezo jeshini (wa kwanza kushoto) na Kaimu mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Alex Nkenyenge (wa kwanza kulia).
IMG_4838
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akipiga gitaa pamoja na bendi ya jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) wakati wa makabidhiano ya Ulingo wa Ngumi uliotelewa na Wizara hiyo kwa jeshi hilo leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Daudi Manongi – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (WHUSM).