NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Ali Kiba Asaini Mkataba na Kampuni kubwa ya Muziki duniani ya Sony jijini Johannesburg, Afrika Kusini

Mwimbaji staa wa bongofleva Alikiba leo amesaini mkataba na  Sony Music , kampuni kubwa ya muziki inayofanya kazi na mastaa wa dunia kama Beyonce, John Legend na Chris Brown.

Moja ya kazi za mkataba huo ni kumtengeneza Alikiba kweye kiwango cha juu zaidi kimuziki, kibiashara na kugharamia video zake na anaporekodi audio zake, kila anapotoa muziki mpya unaachiwa kwa nguvu ya usimamizi wa Sony Music kwenye masoko makubwa ya muziki kama Marekani, Ulaya na Africa.

Mkataba  huo aliosaini Ali kiba unafanana  na ule aliosaini mwimbaji staa wa Nigeria Davido ambapo unavipengele vya kusababisha kolabo kwa urahisi zaidi na mastaa wakubwa wakiwemo wa Marekani.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment