Akiongea
kwenye kipindi cha Friday Night Live, Alikiba almesema wimbo huo
hajamuimbia Jokate na wala hajawahi kumuimbia mtu yeyote, bali aliimba
kwa ajili ya mashabiki wake.
”
Sijamuimbia mtu yeyote kwa kweli, mi nimeimba kwa ajili ya mashabiki
wangu, kwanza sijawahi kumuimbia mtu kabisa, sijawahi, so ni kwa ajili
ya mashabiki wangu”,.
Lakini
pia Alikiba alisema kuwa kitendo cha kuwataja wasanii wa Filamu Wema
Sepetu na Lulu kwenye wimbo huo, ilikuwa ni suprise, hivyo wenyewe
hawakujua kuwa wameimbwa, isipokuwa alishawahi kumdokeza Wema Sepetu
ambaye ametaja kuwa ni rafiki yake mkubwa.
“Wenyewe
walikuwa hawajui kuwa nimewaimba, ila Wema nilimwambia siku moja kuwa
bichwa nina suprise yako, ila Lulu sikuwahi kumwambia na hata sijui
ameipokeaje, ila naamini kaipokea fresh”, alisema Alikiba.
Kitu
ambacho bado kinawapa kigugumizi watu ambao walikuwa wakifuatilia
kipindi hicho, pale aliposhindwa kuchagua kati ya Wema Sepetu na Jokate,
na kusema anawachagua wote, na kuzidi kuweka hali ya sintofahamu kwa
wawili hawa (KIba na Jokate) huenda bado wako pamoja.
eatv.tv
0 comments:
Post a Comment