NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Bodaboda Wagongana Jijini Mwanza, mmoja afariki


Mwendesha pikipiki ambaye hajafahamika amefariki dunia baada kugongana uso kwa uso na mwenzake, eneo la Mabatini jijini Mwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema bodaboda mwingine Stanley Maimu (24), alijeruhiwa katika tukio hilo lililotokea Mei 15.

Msangi alisema ajali hiyo ilisababishwa na mwendokasi wa wahusika, hivyo bodaboda wote walishindwa kumudu pikipiki zao na kugongana uso kwa uso.

Katika tukio jingine, Polisi inawashikilia watu wawili; Chacha Mwita (34) na Rashid Mohamed (34) wakazi wa Kata ya Kitangiri wilayani Ilemela kwa kosa la kukutwa na misokoto sita ya bangi kinyume na sheria.

Kamanda msangi alisema Mei 14 saa 14.00 mchana, polisi waliokuwa doria walifanikiwa kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwapo kwa watu hao wanaojihusisha na biashara hiyo haramu ya kuuza dawa za kulevya.

Aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano wanapobaini vitendo vya uhalifu.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment