NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Katibu Mkuu Chadema Ziarani Ghana


Katibu Mkuu wa Chadema Dk Vincent Mashinji ameanza ziara ya kikazi ya siku tano nchini Ghana ambako pamoja na shughuli nyingine, atashiriki mkutano wa kimkakati kuhusu masuala ya uchaguzi.

Katika ziara hiyo, Mashinji anatarajiwa kukutana na mgombea urais wa chama rafiki na Chadema, New Patriotic Party (NPP), Nana Akufo Addo kwa ajili ya kushauriana, kubadilishana uzoefu wa kisiasa na kupeana mikakati ya ushindi katika uchaguzi.

Dk Vincent Mashinji pia atakutana na Dk Klaus Schuler ambaye ni meneja wa kampeni wa Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel. Dk Schuler pia ni Meneja Mkuu wa chama tawala Ujerumani cha CDU.

Katika ziara hiyo, Dk Mashinji ameambatana na Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri, John Mrema ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita alikuwa meneja wa kampeni wa mgombea urais wa Chadema aliyewakilisha Ukawa, Edward Lowassa.

 Mbali ya Tanzania, nchi nyingine 15 zinazotarajiwa kushiriki mkutano huo ni pamoja na Kenya, Uganda, Zimbabwe, DRC, Angola, Namibia, Nigeria, Senegal, Ivory Coast, Togo, Burkina Faso, Benin, Afrika Kusini, Ghana na Ujerumani.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment