NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

IDDI AZANI (CCM) AJIONDOA KESI YA UBUNGE MAHAKAMANI

mtulia (2)


Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Dar es Salaam, Iddi Azani kupitia wakili wake Abubakari Salim amemuomba Jaji Chochi wa  mahakama katika Mahakam ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini hapa, kufuta shauri la kesi yake aliyokuwa amemshitaki Maulidi Mtulia (CUF) ambaye ndiye Mbunge wa sasa wa jimbo hilo kwa kile alichokuwa akidai kuwa mbunge huyo hakushinda kihalali katika Uchaguzi Mkuu 2015.

Awali akiwasilisha ombi hilo wakili wa Iddi Azani alisema wamefikiria maslahi mapana ya wananchi wa jimbo hilo na hawakuona sababu ya kuendelea na kesi hiyo.

Majibu ya Hakimu Chochi kutoka Mahakama Kuu “Mahakama hii haina nia wala sababu ya kulazimisha kuendelea kwa kesi hiyo, na hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 30, sheria ya mwenendo wa madai ya 33, upande unaoshinda ndio unaostahili kupewa gharama, kwa hiyo nimeruhusu shauri hili namba 3/2015 liondolewe mahakamani kuhusu gharama mtaelewana wenyewe”.

Kwa upande wake Mbunge Mtulia amesema amefurahia uamuzi wa Iddi Azani kwa kutambua umuhimu wa wananchi wa Kinondoni, lakini pia ameeleza kufurahishwa na kitendo cha mahakama kutenda haki.

Katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana Maulidi Mtulia kupitia tiketi ya CUF alitangazwa kuwa Mbunge halali wa Jimbo la Kinondoni kwa kupata kura 67,300 dhidi ya Iddi Azani (CCM) aliyepata kura 65,700.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment