Ndege moja aina ya Airbus A320 ya
Shirika la Ndege la Misri la EgyptAir, iliyokuwa ikitoka Mji Mkuu wa
Ufaransa Paris hadi Cairo, imeripotiwa kupoteza mwelekeo na kupata
ajali mapema leo asubuhi ikiwa na abiria 59 na wahudumu kumi, Maafisa wa Anga wa Misri wamesema.
Hata hivyo Waziri Mkuu wa nchi hiyo
Sherif Ismail amesema bado mapema kutolea ufafanuzi wa ndege hiyo kama
ni suala la kiufundi au shambulizi la kigaidi lililopelekea ndege hiyo
kupata ajali.
Mapema
mwaka huu ndege moja ya Shirika la Ndege la EgyptAir iliripotiwa
kutekwa nyara na kulazimishwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Larnaca
Kusini mwa Pwani ya Taifa la Cyprus.
Ndege hiyo MS181,airbus A320 ilikuwa
imebeba abiria 81 kutoka Alexandria kuelekea Cairo ilitekwa nyara na
mwanaume mmoja aliyekuwa abiria wa ndege hiyo na kutishia kujilipua.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
NGEGE YA EGYPT YATHIBITIKA KUPATA AJALI
Reviewed by Newspointtz
on
16:05:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment