Mapato makubwa ya fedha zinazotokana na mauzo ya haki za matangazo ya
TV , mauzo jezi na mapato ya udhamini wa jezi, wadhamini na ushiriki wa
Champions league umeendelea kuzipa uthamani mkubwa vilabu vya soka
duniani.
Matokeo
yake, wawekezaji ambao waliwekeza kwenye soka katika kipindi cha mika
10 iliyopita sasa wanavuna mapato makubwa hasa katika timu za England.
UEFA imeongeza malipo katika Champions League kwa asilimia 50% kwa
miaka 3 kuanzia msimu wa 2015-16. Fainali ya mwaka huu, itakayochezwa
San Siro jijini Milan, Italy, baina ya vilabu vya Spain, Real Madrid vs
Atletico, kila timu itapata kiasi cha $100 million. Mapato ya Champions League msimu uliopita
Vilabu 20 ambavyo vinaongoza kwa uthamani vina thamani ya wastani wa
$1.44 billion, ongezeko la 24% kuliko ilivyokuwa miaka 20 iliyopita.
Malipo makubwa ya dili za TV, kama mkataba wa miaka wa miaka 3 wenye
thamani ya $7.9 billion baina ya English Premier Keague na Sky Sports na
BTSport ambao unaanza msimu wa 2016/17, na dili nyingine za udhamini wa
jezi, mfano ukiwa mkataba wenye thamani ya $130m kwa mwaka baina ya
Manchester United na Adidas.
Timu
yenye thamani kubwa ya soka kwa mwaka wa nne mfululizo ni Real Madrid
wakiwa na thamani ya $3.65 billion, ongezeko la 12% la thamani
waliyokuwa nayo mwaka uliopita. Wanaowafuatia ni FC Barcelona ambao wana thamani ya $3.55 billion, ongezeko la 12% la thamani kutoka msimu uliopita. Barcelona
huenda wakawapita wapinzani wao kutokana na mkataba wa $400 million la
utengenezaji upya uwanja wao wa Camp Nou, ambao unategemea kukamilika
ndani ya miaka mitano. Timu
ya 3 kwa thamani kubwa ni Manchester United, klabu ambayo ipo kwenye
soko la hisa. Forbes wanaitaja kuwa na thamani ya $3.32billion, ongezeko
la asilimia 7 la thamani kutoka mwaka jana. Man United wametengeneza
faida ya $190m kwa msimu wa 2014-15, kwenye listi hii Man United ndio
timu iliyoingiza faida kubwa kwa upande wa soka lakini wapo nyuma ya
Dallas Cowboys ($270 million) na New England Patriots ($195 million)
kiujumla.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
Listi ya vilabu tajiri duniani, Madrid, Barca zaongoza, Man Utd yaongoza kwa kuingiza faida kubwa
Reviewed by Newspointtz
on
07:58:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment