Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI
Seleman Jaffo amewataka wananchi kutunza miundombinu ya mradi wa Mabasi
yaendayo Haraka (DART) pamoja na mabasi yenyewe ili kuufanya mradi huo
wa kipekee katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki kuwa endelevu.
Naibu Waziri huyo amesema Tanzania
itakuwa ni miongoni mwa nchi zenye maendeleo makubwa baada ya
kukamilisha miradi mikubwa iliyo kwenye mpango ya utekelezwaji, ukiwemo
ujenzi wa barabara za juu ‘fly over’ kwenye makutano ya Barabara za
Nyerere na Mandela ambako harakati za ujenzi zimeanza lakini pia awamu
ya pili ya mradi wa DART utakaohamia Barabara ya Kilwa
itakayowaunganisha wakazi wa Mbagala kabla ya mradi wa tatu utakaowahusu
wakazi wa Gongo la Mboto.
Jaffo
ameyasema hayo baada ya kutembelea mabasi yaendayo haraka yanayotarajia
kuanza kutoza nauli kesho ambapo amewataka watendaji wa DART
kuharakisha mfumo wa ulipaji wa nauli kwa kutumia kadi ili kuepuka
upotevu wa mapato unaoweza kusababishwa na watu wasio waaminifu huku
akiliagiza Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi kuanzia vituoni.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa
UDART David Mgwassa amesema huduma ya mabasi hayo itaanza saa 11:00
alfajili hadi saa 6:00 usiku kwa kutumia mfumo wa tiketi ambazo
zitapatikana katika kila kituo huku wakiendelea kukamilisha mfumo wa
kadi uanaotarajiwa kuanza kutumika rasmi baada ya siku tano.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
MAGARI YA HARAKA KUANZA RASMI LEO
Reviewed by Newspointtz
on
07:14:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment