NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

 

Lile jina alilowahi kubatizwa Mwanamke kuwa ni “PAMBO LA MJI” Kwa sasa imekuwa kinyume na badala yake anaandamwa na majukumu lukuki likiwemo la  Sokoni,  Kupika, Kulima, Ufugaji, Kumuandaa mtoto, Kuteka maji, Usafi, Kumliwaza mume, Kulea, Biashara ndogondogo, Kunyonyesha na mengine mengi.  Hatakama haitawezekana kusaidiwa baadhi ya majuku hayo kwa kigezo cha 50/ 50 basi mwanamke hufarijika anapofanyiwa mambo haya ingawa wanaume wengi huchukulia kawaida.

 Mwanasaikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam  Profesa Chris Mauki kuhusu jambo gani mwanamke hufarijika anapofanyiwa licha ya kuelemewa na majukumu lukuki, ambapo amelitaja swala la Mawasiliano kuwa ni moja ya vitu ambavyo wanawake wanapenda ingawa wanaume wengi wanashindwa kutekeleza hilo suala kwa kuona halina umuhimu.

“Wanawake wanapenda mawasiliano wanapenda uwasiliane wajue uko wapi unafanya nini, na nani, wanaume wengi wakishaulizwa maswali kama haya wanakuwa wakali, kuna mahitaji ambayo wote wanafanana na kuna vile wanavyovipenda kama kuambiwa ukweli lakini mwingine anakataa mimi bora asiniambie”

Wanawake wanapenda ukaribu wa kujali hisia zake, kuzungumza nae kuonyesha unamjali, kuonyesha una muamini na kumpa kipaumbele katika maisha ya kawaida hata kwenye mahusiano, vile vile mwanamke anapenda kujaliwa katika matatizo na kusifiwa pale anapopatia au anapofanya kitu sahihi hii pia ni katika maisha ya mapenzi na hata nje ya mapenzi.

Katika mahusiano mwanamke anapenda kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake kiafya, kihisia na kiuchumi pia mazungumzo ni muhimu kwa sababu mwanamke huumizwa sana na vipindi virefu vya ukimya sio tu kwamba wanataka mazungumzo bali mazungumzo yenye kuleta hamasa katika maisha na yenye mvuto ndani yake, alisema Mauki.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment