Mwigizaji wa filamu Tanzania
Wema Sepetu ametangaza rasmi Application yake 22 May 2016 ikiwa ni njia
rahisi zaidi ya kujiweka karibu na mashabiki wake.
Kupitia mfumo wa APP na SMS utaweza
kupata habari,picha na video clips za maisha ya Wema Sepetu. Uzinduzi wa
APP hii ulihuthuriwa na Waziri wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo Mh
Nape Nnauye.
Application hii itahusisha wale
watumiaji wa simu za Smartphone na hata ambao si watumiaji wa Smartphone
pia,Kama unatumia Smartphone unaweza kudownload Application hiyo kama
zingine tu ila wasio na Simu za Smartphone watajiunga kwa kutuma neno wema kwenda 15404 na watakuwa wanapokea meseji mbili kila siku za matukio yanayomuhusu Wema Sepetu.
Haya ni maelezo ya Wema Sepetu kutoa IG Yake.
“Kwanza
Kabisa nichukue nafasi hii Kusema Asante Mungu wangu kwa kunifanikisha
kukamilisha kile ambacho nimekuwa nikikitamani na ambacho nimefanyia
kazi kwa takribani ya miezi Mitano mpaka kufika siku hii ya leo… Lakini
pia niseme Asante kwa Familia yangu yote kwa ujumla, Bila kusahau
mashabiki wangu wapenzi kwa kunipa moyo wa kutokukata tamaa japokuwa
kuna mengi ambayo kwa binadamu wa kawaida huwezi vumilia Ila kiukweli
mashabiki wangu mmekuwa mnanipa nguvu na Courage everyday… Najisikia
Fahari sana Leo hii kuwa Mwanamke wa Kwanza Barani Africa Kuwa na
MobileApp inayonitangaza mimi Mwenyewe kama Content…. Kwa kutumia hii
App unaweza kupata chance ya kupata zile habari zote za uhakika kuhusu
Wema Sepetu… Kuna vingi ambavyo pia unaweza kupata kama Video Clips,
Audio na Pictures kwa wale watumiaji wa Smart Phone… Lakini pia kwa wale
wasio na Smart phone basi unapata Habari na Matukio mbali mbali kuhusu
mimi ambayo sio Longo longo… Trust me with this app kuna mengi saaana
mtakayoyapata… Ni Rahisi sana Una tuma Neno “Wema” kwenda namba 15404
and u are done…. Asanteni sana…. Nawapenda Mno… Huduma hii ipo
Applicable kwa Mitandao Yote Tanzania…. What are u waiting for…?
Hongera Wema Sepetu.
0 comments:
Post a Comment