NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

MASHABIKI RUSSIA WAWATANDIKA TENA ENGLAND, UEFA KUTOA ADHABU KWA NCHI YAO


Russia itakutana na rungu la Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa) baada ya mashabiki wake kuwashambulia na kuwaumiza wale wa England.

Vurugu kubwa zilitokea wakati wa mechi ya kwanza ya michuano ya Euro 2016 jijini Marseille nchini Ufaransa wakati England na Russia zilipomaliza dakika 90 kwa sare ya bao 1-1.

Mashabiki hao walirusha moto na kupiga bunduki za mwangwi zinazotoa moto wa miale, jambo ambalo Uefa inaona si sahihi.

Mashabiki wa England pamoja na kuonekana au kujulikana ni wajeuri, lakini walilazimika kukimbia kutokana na vurugu hizo ambazo awali zilianza hata kabla ya mechi.






Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment