NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

MADIWANI CHADEMA WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA UCHOCHEZI

court-03

 

Madiwani watatu wa Chadema na mfuasi mmoja wa chama hicho wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Rombo kwa makosa ya kufanya uchochezi.

Madiwani hao, Nicolaus Kimario (Kirio), Anasia Kimario (Viti Maalumu), Daud Tarimo (Leto )na mfuasi wa Chadema, Rogath Kanje walikana mashtaka hayo.Mwendesha mashtaka, Bernard Machivya ameieleza mahakama kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo Agosti 25, wakiwa nyumbani kwa mmoja wa washtakiwa Nicolaus Kimario.

Amedai kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo kwa pamoja wakati wakifanya vikao vya kuhamasisha wananchi wajitokeze kwenye maandamano ya Ukuta Septemba Mosi.

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Rombo, Naomi Mwerinde ameahirisha kesi hiyo hadi Septemba 5 na watuhumiwa wote wataendelea kukaa rumande.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment