SERIKALI imeamua kukata rufaa katika
Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu uliosema kipengele
cha umri wa mtoto wa kike kuolewa chini ya miaka 18 kwamba kinakiuka
Katiba kwa nia ya kuufanya uamuzi huo kuwa sheria.
Uamuzi wa Mahakama Kuu uliitaka
Serikali kufuta vifungu viwili cha 13 na 17 vya Sheria ya Ndoa ya Mwaka
1971 vinavyoeleza mtoto wa miaka 14 na 15 anaweza kuolewa kwa idhini ya
mzazi au Mahakama.
Waziri
wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe alisema kuwa Serikali
imeamua kukata rufaa Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi huo si kupinga
uamuzi wa Mahakama Kuu, bali kupata uamuzi wa chombo cha juu cha
Mahakama ambao hautaweza kubadilishwa na hivyo kuwa kama sheria.
Aliyasema hayo jana Dar es Salaam
alipokutana na Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) ambao
walimtembelea ofisini kwake kuzungumzia mambo kadhaa likiwemo suala hilo
la serikali kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.
Dk Mwakyembe alisema si kwamba serikali
inapingana na uamuzi wa Mahakama Kuu ila kinachofanyika ni utaratibu wa
kawaida ambao utaiwezesha Serikali kuwa na uamuzi kutoka katika chombo
cha juu kabisa cha Mahakama nchini.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
SERIKALI YAPINGA SHERIA YA NDOA
Reviewed by Newspointtz
on
07:24:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment