NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

SERIKALI YAPINGA SHERIA YA NDOA

 

SERIKALI imeamua kukata rufaa katika Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu uliosema kipengele cha umri wa mtoto wa kike kuolewa chini ya miaka 18 kwamba kinakiuka Katiba kwa nia ya kuufanya uamuzi huo kuwa sheria.

Uamuzi wa Mahakama Kuu uliitaka Serikali kufuta vifungu viwili cha 13 na 17 vya Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 vinavyoeleza mtoto wa miaka 14 na 15 anaweza kuolewa kwa idhini ya mzazi au Mahakama.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe alisema kuwa Serikali imeamua kukata rufaa Mahakama ya Rufani dhidi ya uamuzi huo si kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu, bali kupata uamuzi wa chombo cha juu cha Mahakama ambao hautaweza kubadilishwa na hivyo kuwa kama sheria.

Aliyasema hayo jana Dar es Salaam alipokutana na Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) ambao walimtembelea ofisini kwake kuzungumzia mambo kadhaa likiwemo suala hilo la serikali kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Dk Mwakyembe alisema si kwamba serikali inapingana na uamuzi wa Mahakama Kuu ila kinachofanyika ni utaratibu wa kawaida ambao utaiwezesha Serikali kuwa na uamuzi kutoka katika chombo cha juu kabisa cha Mahakama nchini.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment