NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

PICHA 6: NDONDO CUP ILIVYOTOKA USWAZI NA KUTINGA UBALOZI WA CHINA


IMG_0550
Alhamisi August 4, mashindano ya soka la mchangani ‘Ndondo’ yalipiga hatua nyingine baada ya kutoka uswazi na kutinga katika ubalozi wa China nchini Tanzania kwa mwaliko maalum wa chakula cha jioni.

Ubalozi wa China chini ya balozi Dkt. Lu  Youqing ulizialika timu tatu zilizofanya vizuri kwenye mashindano ya Sports Extra Ndondo Cup msimu huu wa 2016.

Timu zilizoalikwa kwenye chakula cha jioni kwenye ubalozi wa Chini ni pamoja na washindi wa tatu wa mashindano hayo Makumba FC, washindi wa pili Kauzu FC na mabingwa wa michuano hiyo Temeke Market.

Timu hizo ziliongonzwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh. Paul Makonda, uwakilishi kutoka shirikisho la soka Tanzania (TFF) na uwakilishi kutoka chama cha soka mkoa wa Dar es Salaam (DRAFA).

Balozi wa China nchini Tanzania amesema, amevutiwa na mapenzi ya soka waliyonayo watanzania hasa kuanzia katika ngazi ya chini licha ya wachezaji kucheza kwenye viwanja vyenye ubora duni lakini bado wanapambana kutimiza ndoto zao.

“Mchezo wa soka ndiyo unapendwa zaidi Tanzania, katika fainali ya Ndondo Cup nimeshuhudia upendo wenu kwenye soka ingawa uwanja wa michezo si mzuri sana lakini haiathiri shauku yenu,” amesema balozi huyo ambaye aliahidi kushirikiana na serikali ya mkoa wa Dar es Salaam chini ya Mh. Paul Makonda kuboresha viwanja vya soka.
IMG_0478 IMG_0482 IMG_0483 IMG_0485 IMG_0490
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment