NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Ufaransa waahidi neema Tanzania

 

BaloziUfaransa

UFARANSA imesema itaongeza mchango wake katika kuendeleza sekta mbalimbali nchini kutoka wastani wa Euro milioni 50 kila mwaka, ambazo huzitoa kupitia shirika lake la maendeleo la AFD.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Maendeleo ya Kimataifa wa Ufaransa, Jean-Marc Ayrault ambaye alifanya ziara nchini na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Augustine Mahiga.

Waziri huyo akiwa nchini pia alifanya mazungumzo na Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli. Katika mazungumzo yake na Dk Mahiga, Waziri huyo alisema uhusiano kati ya Ufaransa na Tanzania uliodumu kwa muda mrefu utaendelea kuimarishwa. 

 Aidha Ayrault aliipongeza Tanzania kwa kuendelea kupigania amani na usalama katika bara la Afrika na hasa juhudi zake za mara kwa mara za kuhakikisha kunapatikana suluhu kwa migogoro ya nchi za Maziwa Makuu.

Aliipongeza Tanzania kwa kukubali kupokea maelfu ya wakimbizi kutoka Burundi na kuwahifadhi na pia mchango wake katika kukabiliana na ugaidi duniani.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment