Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa
nchini, TFDA, imebaini uwepo wa kemikali zinazobakia kwenye mayai ya
kuku na kuku ambao tayari wanaenda kuuzwa ambazo si salama kwa afya ya
binadamu.
Hayo yanebainika wakati wa uzinduzi wa
bodi mpya ya washauri wa TFDA ambapo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, ameiagiza mamlaka hiyo kuchukua
sampuli na kufanya vipimo ili wizara ichukue hatua na kunusuru afya za
watumiaji wa vyakula hivyo.
Katika
hatua nyingine, Mh. Ummy ameiagiza TFDA kutoa ushirikiano kwa
wawekezaji wanaotaka kuwekeza kwenye viwanda vya dawa kwa kuwapatia
wataalam ambao watahakikisha dawa zinazozalishwa nchini zina ubora,
kwani hivi sasa zaidi ya asilimia 85 ya dawa zinanunuliwa nje ya nchi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya
ushauri ambayo inaishauri wizara kutoka TFDA Dkt. Ben Moses amesema
wameyapokea maelekezo ya waziri na watayatekeleza kwa kipindi kifupi
kuanzia leo, hasa suala la usalama wa chakula na dawa kuzingatiwa.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
UMMY awaonya wala kuku na mayai ya kuku
Reviewed by Newspointtz
on
08:23:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment