MKUTANO wa Nne wa Bunge la 11
unatarajiwa kuanza leo mjini hapa, huku miswada sita ukiwemo wa Sheria
ya Upatikanaji wa Habari ukitarajiwa kuchukua nafasi kubwa.
Katika mkutano huo, wabunge wa kambi ya upinzani ambao walisusia siku kadhaa za mkutano uliopita, wamesema kwamba watahudhuria.Mbunge wa Vunjo, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), alithibitisha jana kwamba wabunge wa upinzani wataingia bungeni.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kitengo cha
Habari, Elimu na Mawasiliano ya Bunge kwa vyombo vya habari iliyotolewa
jana, jumla ya maswali 110 yanatarajiwa kuulizwa na wabunge na kujibiwa
na Serikali.
Aidha, Waziri Mkuu anatarajiwa kuulizwa
maswali 16 ya papo kwa hapo. Taarifa hiyo ilisema miswada sita ya
sheria iliyosomwa kwa mara ya kwanza katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na
baadaye kupelekwa katika kamati husika ili ifanyiwe kazi, itaendelea
kushughulikiwa katika hatua zinazofuata ikiwa ni pamoja na kusomwa kwa
mara ya pili, kamati ya Bunge zima na kusomwa kwa mara ya tatu.
Miswada hiyo ni pamoja na ule wa Sheria
ya Upatikanaji wa Habari ya mwaka 2015, Muswada wa Sheria ya Utathmini
na Usajili wa Wathamini wa mwaka 2016, Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya
Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serika wa mwaka 2016.
Pia utakuwepo Muswada wa Sheria ya
Usimamizi wa Wanataaluma wa Kemia wa mwaka 2016, Muswada wa Sheria ya
Taasisi ya Utafiti wa Kilimo wa mwaka 2016 na Muswada wa Sheria ya
Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi ya mwaka 2016.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
BUNGE KUANZA NA MISWADA 6 NA MASWALI 110 KWA SERIKALI
Reviewed by Newspointtz
on
08:59:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment