NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

MBOWE AELEZEA UKUTA ULIVYOVIGHARIMU VYOMBO HIVI VYA HABARI

 Image result for picha ya mbowe

Huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo kikitangaza kuhairisha Maandamano ya nchi nzima yaliyopewa jina la UKUTA, wakidai kuwa viongozi wa Dini wamewaomba wasitishe ili waweze kutafuta suluhu kwa kuzungumza na Rais Magufuli.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe ameeleza kuwa licha ya kuhairisha kwa maandamano ya UKUTA kwa muda wa mwezi mmoja, kumefanyika uonevu kwa serikali kuvifungia vyombo vya habari vya Radio 5, Magic FM na Gazeti la Mseto kwa kile anachodai kuwa vimekuwa zikiripoti habari za UKUTA nidyo maana vimefungiwa.

Hivyo ameeleani vikali kitendo hicho na kueleza kuwa hiyo ni dhahiri kuwa nchi hii haifuati misingi ya haki na sheria, huku akifafanua kuwa imefikia hatua vyombo vya usalama vinaingilia muhimili wa vyomba vya habari na kuwataka kuandika vichwa vya habari wanavyoona vinafaa.

Ambapo amesisitiza kuwa wataendelea kupambana ilikufanikisha kuwa haki inapatikana na kila Mtanzania anaishi kwa amani kwenye Taifa lake.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment