NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Vijana waamasishwa kutuza mazingira

Kila ifikapo tarehe 22 mwezi wa Nne kila mwaka duniani huadhimishwa siku ya utunzaji wa mazingira, vijana washauriwa kutumia ujuzi walionao kujitolea kuyatunza na kuyalinda mazingira kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
Haya yameelezwa na muwakilishi wa Tanzania kutoka taasisi ya World merit (country representative), Rose Mbaga katika ukumbi wa Freedom square uliyopo chuo kikuu cha SUA fakati ya science Mazimbu, Morogoro.
Rose akazungumzia makutano hayo na dhumuni la kuadhimiza siku hiyo ni kuwahamasisha vijana kujitambua nafasi kubwa waliyonayo katika kusimamia na kuyatunza mazingira wakiwa ni nguvu kazi ya taifa.
“kulingana na wingi wa nguvu kazi ya vijana nchini hata duniani hivyo tukaona ni fursa sasa kwa wingi huu wa vijana kuwahamasisha na kuwafanya kuwa kipaumbele katika kuyatunza na kulinda mazingira ili hata wanyama na wadudu watambue uwepo na nguvu za vijana” alieleza Rose.
Amesema kwa kushirikiana na mashirika kama Raleigh Tanzania, Global peace foundation, Economic diplomacy wameadhimia kuwafikia vijana kuwapatia elimu ya utunzaji mazingira kwakuwa nafasi ya utunzaji tegemezi ni vijana wenyewe na kuiita siku hii ni Earthday Tanzania.
Kwa upande wake muwakilishi wa Global peace foundation Tanzania, Kamara Dickson alisema siku ya maadhimisho hayo ni muda muafaka kwa jamii kujitahimini katika matumizi ya rasilimali kwa kizazi cha sasa.
Earth day Tanzania ni wakati mzuri kwa watu kutambua kuwa wao ndio chanzo tegemezi kwa kulinda mazingira kwaajili ya jamii ijayo kunufaika na utunzaji wa sasa, pasipokuwa na usimamizi na utunzaji mzuri hivi sasa hakika vizazi vyetu vijavyo havitoweza kushi kwa muda mrefu” alifafanua Kamara.
Katika kongamano hilo mbali na kuadhimisha siku ya utunzaji wa mazingira duniani vijana wamehaswa kuchangamkia fursa mbali mbali zitolewazo na taasisi za hapa nchini.
Baadhi ya washiriki katika maadhimisho yahayo nao walifurahia nafasi ya vijana kuwa kipaumbele kila sekta pia kutoa pongezi za dhati kwa waandaaji kuwakumbusha vijana nafasi waliyonayo katika jamii.
kupitia mafunzo ya leo nimejifunza vitu vingi mbali na kijana tambua nafasi yao katika kutunza mazingira pia tunapaswa kudhubutu, kwani vijana wengi wamekuwa na maono mengi ila kudhubutu kuyatekeleza mawazo yao imekuwa ni ngumu” alisema mmoja wa waudhuriaji, Theresia Chua.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment