Golikipa wa kimataifa ya Jamuhuri ya Czech Petr Cech ametangazwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa nchi hiyo.
Cech Mwenye umri wa miaka
33,alichaguliwa na makocha, wachezaji na viongozi wa timu kutwaa tuzo ya
nane ya uchezaji bora nchini mwake.Golikipa
huyu amewazidi wachezaji wenzake wa timu ya taifa
Mshambuliaji wa
Sparta Prague David Lafata, na kiungo wa Vladimir Darida anayeichezea
Hertha Berlin.
kipa huyu wa klabu ya Soka ya Arsenal ameichezea timu ya taifa michezo 118 tangu alipoanza soka la kimataifa mwaka 2002.
0 comments:
Post a Comment