NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Serikali ya kijiji cha Kisasida, yaitumbua jipu kampuni ya East Africa Power Poll

NDOA iliyodumu kwa miaka tisa kati ya kampuni ya East Africa Power Poll na serikali ya vijiji vya  Kisasida na Ipungi manispaa ya Singida,umevunjika rasmi baada ya serikali za vijiji hivyo  kudai kwamba kampuni hiyo imejaa ulaghai na hakuna mkataba waliowekeana.
Kampuni hiyo ilikuwa iwekeze katika kuzalisha umeme wa upepo na  iliishalipa fidia yenye thamani ya zaidi ya shilingi 400 milioni kwa wakazi 197, ili  waweze kupisha mradi huo.
Katika mkutano mkuu maalum wa vijiji hivyo ulioitishwa kuzungumzia mstakabali wa kampuni hiyo,iliazimiwa kwa kauli moja kwamba hawaitambui tena. kwa madai licha ya kutokuwa na mkataba,pia hakuna mihtasari wala nyaraka zo zote katika ofisi za vijiji hivyo, inayoonyesha kampuni hiyo imeomba uwekezaji.
East Africa Power Poll
Diwani wa kata ya Mungumaji, Shaban Sato, akizungumza kwenye mkutano maalum wa kujadili uhalali wa kampuni ya East Africa Power Poll kuwekeza katika kuzalisha umeme wa upepo katika kijiji cha Kisasida.Pamoja na mambo mengine,diwani huyo aliagiza watu waliolipwa fidia kupisha mradi wa umeme wa upepo,warejee kwenye maeneo yao kwa madai kampuni ya East Africa Power Poll haina mkataba na kijiji hicho.
Aidha, kampuni hiyo imeagizwa isimamie yenyewe zoezi la kurejeshewa fedha za fidia kwa watu waliowalipa,na kwamba serikali za vijiji hivyo,hazitahusika kwa lolote lile.
Mwenyekiti wa kijiji cha Kisasida, Hamisi Rupia,alisema kuwa baada ya kuingia madarakani na kubaini kampuni hiyo haina mkataba na vijiji hivyo wa kumilikishwa hekta 1,450,desemba 23 mwaka jana,aliiandikia barua  ifike ofisini kwake,ili waweze kuzungumzia uhalali wa umiliki huo.
“Lakini hadi hivi sasa,kampuni hiyo haijawahi kujibu baraua hiyo,wala haijawahi kutuma mwakilishi kuja kuelewana na viongozi wa serikali hizi mbili juu ya umiliki wa eneo wanalolitaka kwa uwekezaji wao”,alisema mwenyekiti wa kijiji cha Kisasida.
Diwani wa kata ya Mungumaji (CCM),Shabani Satu,alipigilia msumari kampuni hiyo kwa kudai kampuni hiyo imejaa ulaghai mtupu,na kuagiza watu ambao wamelipwa fidia na kuyahama maeneo yao,warejee mara moja na kuanza shughuli za kibinadamu.
Hamisi Rupia
Mwenyekiti wa kijiji cha Kisasida manispaa ya Singida, Hamisi Rupia,(wa nne kutoka kulia) akizungumza kwenye mkutano maalum uliokuwa na ajenda moja ya mstakabali wa uwepo wa kampuni ka East Africa Power Poll iliyokuwa iwekeze katika kuzalisha umeme wa upepo.
Diwani huyo ambaye huko nyuma aliwahi kuwa mtetesi mkubwa wa kampuni hiyo na kusimamia zoezi la kuorodhesha wakazi wanaostahili kulipwa fidia,alisema kwa kipindi cha miaka tisa,ameshindwa kabisa kuielewa vizuri kampuni hiyo kutokana na mwenendo wake,hivyo kwa watu waliolipwa fidia,watajuana wao na kampuni hiyo.
Kwa upande wake Ramadhani Yusuph,alisema kwamba kwa vile ofisi za serikali za  vjijiji hazina kumbukumbu ya mihtasari yo yote wa mikutano mikuu ya vijiji hivyo inayoonyesha kuridhia uwekezaji wa hekta 1,450,kitendo hicho pekee,kinainyima sifa kampuni hiyo kuwekeza.
“Kama kweli wana nia ya dhati kuja kuzalisha umeme wa upepo kwenye maeneo yetu,sisi hatuwezi kupigana na uwekezaji wa kitaifa.Waje waanze upya kuomba kwa kuzingatia taratibu na sheria zilizopo”alisema.
Naye Maulidi Simba,alisema fedha ya fidia aliyolipwa,haikuwa halali …..ni ndogo sana tena ni ya kununulia bajia tu.Hivyo ameitaka kampuni hiyo kumlipa fidia stahiki kwa kumsimamisha kuendelea na shughuli za uzalishaji kwa kipinid cha zaidi ya miaka tisa.
East Africa Power Poll
Juma Maluja, akitoa nasaha zake mbele ya mkutano mkuu maalum ulioitishwa kujadili uhalali wa kampuni ya East Africa Power Poll kuwekeza kijijini hapo kwa ajili ya kuzalisha umeme wa upepo.
Akizungumzia sakata hilo, Afisa ardhi mteule manispaa ya Singida,Christian Kasambala,alisema kuwa mgogoro huo ulioibuka upya,kwa kiasi kikubwa unachangiwa na wanasheria wa vichakani, ambao ni wapotoshaji wakubwa.
“Maombi ya uwekezaji ngazi ya kitaifa,hayatumwi au hayaombwi katika ngazi ya  serikali za vijiji, serikali za vijiji hazina ardhi…ardhi inamilikiwa na mtu mmoja mmoja. Kisheria maombi hayo yanatumwa  katika ngazi ya halmashauri na nakala inapelekwa wilayani na mkoani.Hivyo ndivyo kampuni ya Power Poll ilivyofanya”alifafanua.
Akifafanua,Kasambala alisema wakati wa kulipa fidia walengwa wote walielimishwa taratibu na sheria zilizofuatwa katika kufikia kila kiwango cha fidia kwa mhusika.Wote  walikubaliana na hatua hiyo na kupokea fidia kwa roho nyeupe na kusaini kwenye daftari.Amedai fidia hiyo ililipwa katika ofisi ya Mkuu wa wilaya.
Imeandaliwa na Nathaniel Limu, Singida
East Africa Power Poll
Baadhi ya wakazi wa kijiji cha 


Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment