WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema serikali iko kwenye mpango
kabambe wa kulifufua Shirika la Ndege la Taifa la Tanzania (ATCL) ili
kuiwezesha nchi kumiliki ndege zake kama awali na kwamba watumishi ambao
walibainika kulihujumu kamwe hawatapata nafasi tena ya kutumika.
Alisema mpango uliopo kwa sasa ni kuanza na ununuzi wa ndege mpya mbili ili kulipa uhai shirika.Aliyasema
hayo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani hapa iliyolenga kukagua
shughuli za Uwanja wa Ndege wa Tanga na idara nyingine za wizara hiyo
zikiwemo Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
(TAA) na Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA).
“Kwa kuwa tayari fedha ipo
na imeshatengwa kwa ajili ya ndege hizo, hatua inayoendelea sasa ni
kuzungumza na wataalamu na iwapo tutakubaliana basi Air Tanzania itaanza
kufanya kazi kwa kasi mpya,” alisema.
Aliongeza kuwa, uwepo wa ndege mbili
ina maana kwa siku kutakuwa na uwezekano wa wastani wa kusafiri safari
nyingi zaidi katika maeneo mbalimbali nchini, yakiwemo yenye vivutio vya
utalii. Aidha, amewataka watanzania kuwa wazalendo kwa kutumia usafiri
wa ndege hizo za serikali.
Akizungumzia ilivyojipanga kukabili
hujuma ambazo zimetajwa kuliathiri shirika, alisema Air Tanzania mpya
haitaajiri watumishi ambao kumbukumbu zao za ajira zinaonesha walifanya
madudu ndani ya shirika hilo.
“Tayari wizara inao
mwongozo. Tutawaondoa watumishi wote wabovu ambao walihujumu shirika ili
kutoa fursa ya kuanza upya na wale ambao walikuwa wazalendo katika
kutimiza majukumu yao ya kazi kwa maslahi ya watanzania na taifa kwa
ujumla.
“Kuna wale wapiga dili,
taarifa zao ninazo na ninawajua hivyo wasitegemee kabisa kubaki
tutakapofufua shirika. Ni afadhali tukawa na watu hata kumi, lakini
wachapa kazi na wazalendo kuliko kuwa na watu wahuni ambao wanajali
maslahi yao binafsi,” alisisitiza.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
SERIKALI YAWEKA MKAKATI WA KUFUFUA ATCL
Reviewed by Newspointtz
on
12:38:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment