Chama
cha Wanasheria Wanawake nchini (TAWLA) kimetoa mafunzo kwa waandishi wa
habari yanayolenga kujenga uelewa kwa waandishi wa habari kuhusiana na
masuala ya haki ya afya ya uzazi, changamoto wanazokutana nazo na namna
ambavyo matumizi ya sheria za kimataifa zitaweza kupunguza chanagamoto
hizo.
Afisa
Uchechemuzi wa Shirika la Wanasheria wanawake la TAWLA Bi. Sime
Bateyunga akifungua mafunzo kwa wanahabari hawapo pichani yanayolenga
kujenga uelewa kwa waandishi wa habari kuhusiana na masuala ya haki ya
afya ya uzazi, changamoto wanazokutana nazo na namna ambavyo matumizi ya
sheria za kimataifa kama Maputo Protocal yataweza kupunguza changamoto
hizo, Semina hiyo ya siku mbili ilikuwa ikifanyika Luther House Azania
Front jijini Dar es salaam na imemalizika leo.(PICHA NA JOHN
BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Wanahabari
wakimsikiliza Afisa Uchechemuzi wa Shirika la Wanasheria wanawake la
TAWLA Bi. Sime Bateyunga wakati akifungua semina hiyo jana.
Dk. Ali Said kutoka muhimbi akiwasilisha mada katika mafunzo hayo kuhusu utoaji mimba usio salama na madhara yake.
Afisa
habari na mawasiliano TAWLA, Goodness Mrema akiwa katika picha ya
pamoja na baadhi ya waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa
semina hiyo leo.
Afisa
Mipango wa TAWLA, Bi. Sara Kinyaga kulia akiwa katika picha ya pamoja
mara baada ya kuendesha mafunzo hayo kwa waandishi wa habari leo.
Maofisa
wa TAWLA pamoja na waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja
mara baada ya kumalizika kwa semina hiyo leo jijini Dar es salaam.
0 comments:
Post a Comment