Afisa mtendaji Kata ya Mahenge Mjini Rajabu Hussen Mgululi |
MAHENGE-ULANGA
Na.Timotheo Lupembe
Ofisi ya kata ya Mahenge Mjini imefanikiwa kuodoa
kero ya Madawati 135 katika Shule mbili za Msingi na Moja ya Sekondari katika
Kata hiyo.
Akizungumza na newspointtz.blogspot.com
Ofisini kwake Afisa mtendaji kata ya Mahenge Mjini Bwana Rajabu Mgululi amesema ofisi yake
kushirikiana na wadau wa maendeleo wamehakikisha zoezi hilo linafanikiwa kwa haraka
ili kuondoa kero hiyo kwa wanafunzi.
Aidha Bwana Mgululi ametaja Shule hizo ni Shule ya
Msingi Mahenge Mjini Madawati 23,Shule ya Msingi Mahenge B Madawati 60 na shule
ya Sekondari Mahenge 52 ambpo mpaka sasa jumla ya Madawati 68 kati ya 135 yamekamilika na kukabiziwa
huku Madawati 67 yakiendelea kutengenezwa.
Pia alisema upatikanaji wa pesa ni changamoto kubwa
ambayo Ofisi ya Kata inapitia ili kutatua kero mbalimbali za kijamii na hilo
wamelifanikisha na ongezo la pesa kutoka kwa wadau wa maendeleo ambao ni
Wafanya Biashara
Hata hivyo Bwana Mgululi ametoa ushauri kwa wazazi
kuwapeleka watoto wao Shuleni kwani kero ya upungufu wa Madawati Ofisi ya Kata
kushirikiana na wadau wa maendeleo wameitatua kwa kiasi kikubwa
0 comments:
Post a Comment