Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wametakiwa kuwa wabunifu katika sehemu zao za kazi ili kuongeza ufanisi katika majukumu yao ya kila siku.
Akitoa
wito huo wakati akifungua Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri
Mkuu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu,Bunge, Ajira,Kazi
na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema watumishi wanatakiwa
kutumia rasilimali walizonazo kuonesha ubunifu wao katika idara na
vitengo walivyopo ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao wa kazi wa
kila siku.
“Ofisi
ya Waziri Mkuu ni mratibu na msimamizi wa shughuli za kila siku za
Serikali hivyo basi naomba tuwe wabunifu katika sehemu zetu za kazi ili
tumsaidie Mhe. Waziri Mkuu kutelekeza majukumu haya kwa kasi na ufanisi
unaotakiwa.” alisema Mhe. Jenista.
Mhe.
Jenista Mhagama ametoa wito kwa wakuu wa Idara na Vitengo kushirikiana
na watumishi katika ofisi zao ili kuongeza ufanisi wa kazi za kila siku
katika idara na Vitengo mbalimbali.
Akizungumza
mara baada ya kikao Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu
Dkt Hamis Mwinyimvua amesema kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi ni
fursa muhimu kwa wafanyakazi kukutana na kujadili masuala mbalimbali ili
kupata mbinu za kupambana na changamoto zinazokabili Idara na vitengo
mbalimbali.
Kwa
mujibu wa Waraka wa Rais Namba 1 wa Mwaka 1970, moja ya madhumuni ya
kuanzishwa kwa Mabaraza ya Wafanyakazi ni kuongeza ufanisi na tija
katika sehemu za kazi na kupitia Mabaraza haya, wafanyakazi pamoja na
waajiri hupata fursa ya kubadilishana mawazo na kubuni mbinu mbalimbali
za kukabiliana na changamoto katika sehemu zao za kazi.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu)
Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akitoa ufafanuzi wa masuala ya wafanyakazi wa
Ofisi hiyo wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya
Waziri Mkuu Aprili 9, 20 katika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri
Mkuu.
Baadhi
ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri
Mkuu wakifuatilia hoja za Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,
Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo
pichani)) wakati wa mkutano wa baraza hilo tarehe 9 Aprili, 2016 katika
Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamis Mwinyimvua
akizungumza wakati wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aprili
9, 2016. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,
Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb).
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu)
Mhe. Jenista Mhagama (wanne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja
na Viongozi na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi hiyo mara baada
ya ufunguzi wa mkutano huo Aprili 9, 2016. (Picha Zote na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
0 comments:
Post a Comment