Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati) akijadiliana jambo na Mkuu wa Kivuko cha Magogoni (kushoto) na Nahodha wa kivuko hicho (kulia) wakati alipokikagua. |
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amefanya
ukaguzi katika kivuko cha Magogoni na kukagua ujenzi wa Flowmeter katika
daraja la Kigamboni ambalo linataraji kuzinduliwa hivi karibuni. Mo
Blog imekuandalia picha za tukio hilo.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto)
akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Kivuko cha Magogoni Eng. Charles wakati
alipokikaga kivuko hicho.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akipanda kukagua mtambo wa kupima na kusafirisha mafuta Flow Meter uliojengwa Kigamboni eneo la Mji Mwema utakaoanza kutumika mwezi Mei.
Meneja
wa mradi wa Ujenzi wa Flow Meter ya Kigamboni Eng. Mary Mhayaya
akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa
Makame Mbarawa alipokagua maendeleo ya ujenzi huo.
Muonekano wa Flow Meter mpya ya Kigamboni katika hatua za mwisho za ujenzi wake.
Muonekano wa Daraja la Kigamboni mara baada ya ujenzi wake kukamilika.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akipata
maelekezo kwa Mkurugenzi Msaidizi Barabara za Mijini Eng. Hussein
Mativila (kushoto) alipokagua Daraja la Kigamboni.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiongea na
Msimamizi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni Kutoka Mfuko wa Hifadhi ya
Jamii (NSSF), Eng. Karim Mattaka wakati alipokagua daraja hilo.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati)
akijadiliana jambo na Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abel
Muhanga (kulia), wakati alipokagua Bandari ya Malindi.
0 comments:
Post a Comment