32FF626D00000578-3531354-image-a-49_1460206736457
Mchezo wa mapema leo Jumamosi wa Ligi Kuu ya Uingereza kati ya West Ham United iliyoikaribisha Arsenal umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya goli tatu kwa tatu.

Arsenal ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata goli kupitia Mesut Ozil dakika ya 18 na baadae Alexis Sanchez kuongeza la pili ambapo baada ya hapo Andy Carroll aliisawazishia timu yake magoli yote mawili dakika ya 44 na 45 na wakaenda mapumziko wakiwa wamefungana goli mbili kwa mbili.

Kipindi cha pili katika dakika ya 52, Andy Carroll kwa mara nyingine aliongeza goli la tatu kwa upande wa West Ham na baadae dakika ya 70, Laurent Koscielny akaifungia goli la tatu Arsenal na mchezo huo kumalika kwa sare ya goli tatu kwa tatu.

Baada ya matokeo hayo, Arsenal imefikisha alama 59 ikiwa katika nafasi ya tatu na West Ham kufikisha alama 52 ikiwa nafasi ya sita ya msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.