Mwanamuziki
mahiri kutoka nchini Marekani Neyo amewasili jijini Dar es Salaam usiku
huu tayari kutumbuiza katika tamasha kubwa la Jembeka Festival 2016
litakalofanyika jijini Mwanza siku ya Jumamosi Mei 21 mwaka huu katika
viwanja vya CCM Kirumba ambapo msanii wa kimataifa nchini Diamond
Platnumz atapanda katika jukwaa hilo sambamba na wasanii wengine wa hapa
nchini watakaosindikiza tamasha hilo.
Tamasha
la Jembeka Festival 2016 limeandaliwa kwa udhamini wa Kampuni ya simu
za mkononi Vodacom, Fastjet, SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK
Security, Samsung, EF Outdoor, Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe FM.
Mwanamuziki
mahiri kutoka nchini Marekani Neyo mara baada ya kuwasili katika uwanja
wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere usiku huu akiwa
amefuatana na Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu (tisheti
nyekundu) pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi wa Tamasha la
Jembeka Festival 2016, Costantine Magavilla (tisheti nyeupe).
Msanii kutoka nchini Marekani Neyo akielekea kwenye usafiri maalum alioandaliwa.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Jembe FM ya jijini Mwanza ambao ndio waandaaji wa Tamasha
la Jembeka Festival 2016, Dr. Sebastian Ndege akiongozana na mmoja wa
wageni walioambatana na msanii Neyo mara baada ya kuwasili kwenye hoteli
ya Hyatt Regency-The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki
Neyo akiwasili kwenye hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, The
Kilimanjaro na kupokelewa na Meneja wa Hoteli hiyo, Timothy Mlay (mwenye
suti nyeusi).
0 comments:
Post a Comment