WABUNGE wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, wamewaomba maaskofu na mashehe
kusaidia kumshauri Rais John Magufuli akubali kuruhusu vyama vya siasa
kufanya mikutano ya hadhara.
Walisema endapo viongozi hao wa dini,
watafanikiwa katika ushawishi wao, nchi itaepuka uwezekano wa kuingia
kwenye machafuko kutokana na utekelezaji wa Operesheni Ukuta
waliyotangaza kuanza Septemba Mosi mwaka huu.
Akizungumza
kwa niaba ya wabunge wa Chadema wa Kanda ya Kaskazini, Mjumbe wa Kamati
Kuu ya Chadema, Godbless Lema, alisema ni viongozi wa dini pekee ndio
wanaweza kusaidia kumshauri Rais Magufuli ili vyama vya siasa,
viruhusiwe kufanya mikutano ya hadhara.
Alisema msimamo wa wabunge wa Chadema
wa Kanda ya Kaskazini ni kufanya mikutano kuanzia Septemba Mosi ili
kudai uhuru wa vyama vya siasa wa kufanya mikutano ya hadhara na
maandamano, kama njia ya kukuza demokrasia nchini.
“Wakati bado tunasuguana sisi na vyombo
vya dola, tunawaomba viongozi wetu wa dini maaskofu, mashehe na
wachungaji wamshauri Rais wetu ili atuachie uhuru huu ambao ni wa
kikatiba ,” alisema Lema.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
LEMA- VIONGOZI WA DINI MSHAURINI JPM,LABDA ATAWASIKIA
Reviewed by Newspointtz
on
08:25:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment