NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

UTAJUAJE KAMA ANATAKA KUKUPIGA KIBUTI

Kila lenye mwisho basi lilikuwa na mwanzo wake, na dalili ya mvua ni mawingu ingawaje baadhi ya wakati inaweza kunyesha bila ya hata kuonekana mawingu, kwenye upande wa mapenzi zipo dalili za kuachwa au kuachika.black couple-fight1.Mwenza kukosa raha mnapokuwa pamoja, mara nyingi unapokuwa nae karibu anakosa furaha na hii ni kutokana na kutokuhitaji uwe nae karibu.

2.Kutopenda kutembelewa ikiwa mnakaa sehemu tofauti au kukutaka utowe taarifa kabla ya kumtembelea, kama ulikuwa una tabia ya kwenda kwake bila kumtaharifu, maisha yatabadilika na kuhitaji taarifa kabla ya kwenda kumuona.

3. Kutoipa umuhimu mitoko yenu kama ilivyokuwa awali, mara nyingi hatokuwa akihitaji kuwa karibu na wewe na mitoko ya awali haitokuwepo na hatakuwa ahishiwi visingizio kila ukitaka mtoke.

4. Kuanzisha majibu ya mkato, tofauti na awali ataanza kukujibu majibu yasiyokupendeza wakati mwingine anaweza akaa kimya kabisa bila kukujibu au akakujibu kwa  mkato. 5.Kutozijibu meseji zako kwa wakati tofauti na ilivyokuwa awali, mawasiliano yenu yatapungua kwa asilimia kubwa na hii sio kwa meseji tu wakati mwingine hata kupokea simu inaweza ikawa ni tatizo.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment