NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

UTUNDU WA MAANDALIZI YA TENDO LA NDOA

 Image result for picha za wapenzi

Ni vizuri utambue kuwa unapoamua kufanya tendo la ndoa ni vyema ukajua mahitaji ya mwenzio iwe mwanaume/mwanamke, jaribu kumfanyia mwenza wako vitu vya tofauti na alivyovizoea ama ambayo anatarajia kuviona kwako kutokana na mazoea. Ukifanya hivyo utamfanya aendelee kuwa na hamu ya kuwa na wewe kwa muda mrefu.

Naweza kusema mwacheni Mungu aitwe Mungu. Mara nyingi mtoto anapozaliwa kuna baadhi ya vitu huwa anafundishwa lakini baadhi ya vitu huwa havihitaji kufundishwa. Kwa mfano hakuna mtu anayemfundisha mtoto kulia, kunyonya, kujisaidia, kucheka, kulala.

Japo kuna baadhi ya vitu ambavyo pindi akikua atatakiwa kuachana navyo na kufanya vya kiutu uzima kama suala la kujisaidia. Kwa sababu yeye hujisaidia ndani ya nguo yake ama popote pale, hivyo hufika muda akaelekezwa jinsi ya kujisaidia kuliko salama. Ndivyo hivyo na katika ndoa.

 Hakuna mtu aliyewahi kufundishwa jinsi ya kufanya tendo la ndoa. Wewe hapo ni shahidi, lakini kuna baadhi ya vitu hulazimishwa kufundishwa kulingana na mazingira husika. Ndiyo maana kuna baadhi ya makabila kuwafunda watoto wao kabla ya kuingia katika masuala ya ndoa.

Hivi ni baadhi ya vitu ambavyo vinaweza kukusaidia katika kuifanya ndoa yako iwe imara ya yenye furaha wakati wote;

A. Uwe mbunifu wa kuangalia ni sehemu ipi ukimshika mke/mumeo anasisimka.

B. Ujue mwili wako na wa mpenzi wako kwa kila mmoja wapi aguswe ili asikie raha.

C. Mweleze mwenzako sehemu ambazo unapenda awe anazichezea ili akupe hisia zaidi.

D. Jiamini katika kutafuta mitindo ambayo itakuwa faida kwa ndoa yenu.

E. Kila mmoja awe wazi kwa mwenzake na ushirikiano wa mpenzi yenu uwe mzuri.

F. Ujue sehemu za kumsisimua kwa utundu na ufundi wako mwenyewe.

G. Muulize sehemu anazopata msisimko ili uzifanye naye asike raha wakati wa faragha.

H. Yajue yanayomkosesha raha ya kufurahia tendo la ndoa.

I . Yajue mambo yanayomletea hisia haraka za kufanya mapenzi.

Jiunge nasi

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment